The House of Favourite Newspapers

YANGA YAPIGWA NA AZAM, ZAHERA AMFUNGUKIA NDEMLA

TIMU ya Azam FC leo Jumanne, Mei 28, 2019 wamelipa kisasi baada ya kuifunga Yanga Sc kwa mabao 2-0, mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Tanzania bara uliopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

 

Bao la kwanza limefungwa na Daniel Amouh dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza na bao la pili limefungwa na Mudathir Yahya dakika ya 50.

 

Timu zote mbili zilikuwa zinatafuta heshima kwenye uwanja wa Taifa leo ikiwa ni mchezo wa mwisho kwa msimu huu baada ya Yanga kuifunga Azam bao 1-0 katika mchezo wa kwanza.

 

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amesema; “Said Ndemla hayupo kwenye makaratasi yangu sina habari zake.”

“…….Hii t.Shirt na kofia zimekuwa ni utambulisho wangu msimu huu bahati mbaya hatujapata ubingwa,msimu ujao ntakuja na muonekano mwengine,“

Comments are closed.