The House of Favourite Newspapers

Rais Magufuli Apokelewa kwa Shangwe Zimbabwe – Video

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Pohn Pombe Magufuli amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Mugabe Jijini Harare nchini Zimbabwe na kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Dambudzo  Mnangagwa.

Magufuli amewasili Zimbabwe leo Jumanne, Mei 28, 2019, akitokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako nchini Namibia baada ya kumaliza ziara yake rasmi ya Kitaifa ya siku mbili nchini humo.

Akiwa nchini Zimbabwe, Magufuli atafanya ziara rasmi ya Kitaifa ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Emmerson Mnangagwa.

Rais Magufuli akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Robert Mugabe Jijini Harare nchini Zimbabwe.

 

MAGUFULI ALIVYOWASILI ZIMBABWE

Comments are closed.