Rais Magufuli Apokelewa kwa Shangwe Zimbabwe – Video
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Pohn Pombe Magufuli amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Mugabe Jijini Harare nchini Zimbabwe na kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Dambudzo Mnangagwa.
Magufuli amewasili Zimbabwe leo Jumanne, Mei 28, 2019, akitokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako nchini Namibia baada ya kumaliza ziara yake rasmi ya Kitaifa ya siku mbili nchini humo.
Akiwa nchini Zimbabwe, Magufuli atafanya ziara rasmi ya Kitaifa ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Emmerson Mnangagwa.
Rais Magufuli akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Robert Mugabe Jijini Harare nchini Zimbabwe.
Comments are closed.