Zari Athibitisha Kuwa Hajarudiana na Diamond
MPENZI wa zamani wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kupitia akaunti yake ya Snapchat amethibitisha taarifa kuwa yeye na Diamond hawajarudiana bali wameelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.
Tangu wiki iliyopita kulikuwa na tetesi zilizodai kuwa Diamond na Zari wamerudiana baada ya wawili hao kuonekana pamoja nchini South Africa na watoto wao.
Zari amefungukia tetesi hizo na kusema yeye na Diamond hawajarudiana kuwa wapenzi bali wameamua kuelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.
Zari amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Snapchat ambapo aliandika:
Tetesi za Diamond na Zari kurudiana zilianza baada ya wawili hao kukutana nchini South Africa baada ya kutoanana kwa miezi minne baada ya kuachana.
Comments are closed.