(Pichaz) Nuruelly na Producer Lessar wafunika Global Tv online
Nuruelly Mbowe ‘Nuruelly’
mtayarishaji Eddy Lessar
Msanii mkali na nguli wa miondoka ya RNB, Bongo, Nuruelly Mbowe ‘Nuruelly’ pamoja na mtayarishaji Eddy Lessar anayefanya vizuri kwenye gemu, leo wamefunika mbaya katika mahojiano na Global TV Online katika ofisi za Global Publishers zilizopo Bamaga-Mwenge, jijini Dar.
Ambapo waandishi wa Global walipandwa na mzuka kwa uimbaji wa Nuruelly na kuomba waimbiwe nyimbo kibao ikiwamo Umetutoka Baba, Tumeagizwa Upendo, Nzela na nyinginezo.
Nuruelly ambaye anafanya kazi na B Bendi ameachia nyimbo zake mbili ikiwemo ya Upendo na Wakati Ndiyo sasa ambazo zimetengenezwa na mtayarisha Eddy Lessar.
Na Gabriel Ng’osha/GPL