The House of Favourite Newspapers

Vyakula vinavyoongeza afya mwilini

0

TIKITIMAJI.jpgVyakula vinavyowafanya wenye afya nzuri kuendelea kuwa nayo  zaidi na wenye afya mbovu, kuwa na  nzuri ni hivi vifuatavyo.

MAHARAGE YA SOYA: Faida yake ni kushusha shinikizo la damu, kuimarisha sukari mwilini, kupambana na ugonjwa wa kisukari, figo, moyo, kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa kansa ya kibofu na magonjwa mengine ya wanawake.

SAMAKI: Wana virutubisho aina ya Omega 3 ambavyo huulinda moyo dhidi ya maradhi, humuongezea mlaji uwezo wa kukumbuka memory, kuna virutubisho vyenye uwezo wa kupambana na kansa mwilini, kuongeza kinga mwilini na kuondoa mafuta mabaya mwilini bad cholesterol.Pia wana virutubisho muhimu kama vile vitamini D, vitamin 12, vitamini B3, vitamini B6, Omega 3 Fatty acids, protini na madini mengine mengi.

KAROTI: Miongoni mwa faida nyingi za karoti mbichi au zilizochemshwa ni pamoja na kushusha kolestro mbaya mwilini, kupunguza unene, kuimarisha nuru ya macho, kuimarisha shinikizo la damu, inatoa kinga kwenye figo na inaimarisha sukari mwilini.

PAPAI, TIKITIMAJI: Ni matunda muhimu mwilini ambayo hata mgonjwa wa kisukari anashauriwa kuyala kwani yana kiwango kikubwa cha ufumwele fibre, huimarisha kiwango cha sukari mwilini. Kula moja katika ya matunda hayo mawili, kila siku.

KITUNGUU SAUMU: Husaidia kuyeyusha damu mwilini hivyo kumuepusha mlaji kushikwa na ugonjwa wa moyo pamoja na presha, pia hutoa kinga kwenye ini na huondoa maumivu ya viungo. Kula angalau kitunguu kimoja mara moja kwa wiki.

TANGO: Husaidia kusaga chakula tumboni hivyo kumuwezesha mlaji kupata choo laini pia linaweza kutumika katika kuboresha ngozi ya uso kwa kupaka na huondoa vipele na kuifanya ngozi kuwa nyororo. Ni zuri linapoliwa na maganda yake na unaweza kula kiasi utakachoweza. Pia kula asali na tende na habari zake tulishaandika kwa kirefu katika safu hii.

Leave A Reply