Ubalozi wa Kuwait Watatua Shida ya Maji Kwa Wanafunzi 5600 Dar
DAR ES SALAAM: Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jasem Al-Najem amezindua mradi wa visima vya maji kwa ajili ya kusaidia wanafunzi 5600 wa shule tatu za msingi Yombo jijini Dar es Salaam.
“Tunashukuru sana kuwa hapa, ni furaha yetu mradi wetu umekamilika, tuna imani utasaidia wanafunzi wengi pamoja na kujenga mazingira mazuri kwa ajili ya kujisomea. Kwa hiyo kama ubalozi tumedhamilia kusaidia shule mbalimbali kama tulivyofanya hapa ili kuboresha elimu,” alisema balozi huyo.
Aidha katika uzinduzi huo msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto alikuwa kivutio kikubwa kwa wanafunzi hao.
Kwa upande wa Mrisho Mpoto ambaye alizungumza kuhusu uzinduzi huyo, aliwataka wanafunzi kutumia vizuri mazingira hayo kwa manufaa yao.
“Kila mwanafunzi hapa ana ndoto yake, mimi ningependa mtumie vizuri haya mazingira, kwa sababu kuna wanafunzi wengine wanatamani mazingira haya ila wanayakosa, kwa hiyo ni vyema mkayatunza na kuyalinda ,” alisema Mpoto.
GABRIEL NG`OSHA/GPL
Comments are closed.