VIDEO: Uwoya Amwaga Pesa Kwa Waandishi, Aahidi Mazito!
MWIGIZAJI wa Bongo Muvi, Irene Uwoya, ameonyesha jeuri ya pesa kwa kuwamwagia pesa waandishi wa habari waliojitokeza katika ukumbi wa Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam leo kwenye mkutano ulioitishwa na wasanii wa Bongo Muvi.
Mkutano huo ulioitishwa na wana-Bongo Muvi wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Steve Nyerere, una lengo la kuzungumzia uzinduzi wa Swahiliflix ambao ni mtandao wa kuuzia muvi, unaotarajiwa kufanyika tarehe 31, mwezi huu mwishoni.
Comments are closed.