The House of Favourite Newspapers

Airtel fursa yaendelea kukwamua vijana hapa nchini‏

0

Mkufunzi kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Tanga,Hassani Juma Hassani akitoa mada wakati wa semina ya Airtel Fursa ilivyofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa YDCP mkoani Tanga.

Meneja mauzo wa Airtel Mkoa wa Tanga, Aluta Kweka akizungumza na wauzaji wa bidhaa za kampuni hiyo wakati wa semina ya Airtel Fursa ilivyofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa YDCP mkoani Tanga.

Meneja mauzo wa Airtel Mkoa wa Tanga,Aluta Kweka akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga kuhusu semina ya Airtel Fursa iliyofanyika kwenye ukumbi wa YDCP mkoani Tanga.

Wafanyabishara wadogo na wa kati zaidi ya 300 waliopo katika wilaya mbali mbali mkoani Tanga wameongezewa ujuzi wa elimu ya biashara ili waweze kufanya shughuli zao kwa ufanisi na kuweza kuongezaza kipato chao na kuchangia pato la taifa.

Kampuni ya Airtel Tanzania, kupitia mpango wake wa “Airtel Fursa Tunakuwezesha” imewapatia mafunzo ya ujasiriamali vijana wa manispaa ya Tanga kwa lengo la kuwawezesha kuboresha uendeshaji biashara na kukuza mitaji yao katika warsha iliyofanyika katika ukumbi wa YDCP uliopo mkoani hapo.

Akifungua warsha hiyo, meneja mauzo wa Airtel mkoa wa Tanga Aluta Kweka katika alisema, “lengo letu hasa ni kuwapatia ujuzi vijana wajasiriamali wenye umri wa kuanzia miaka 18 hadi 24 ili waweze kufanya biashara kwa tija badala ya kufanya kwa mazoea. Mafunzo haya tunataraji yataongeza tija ya kibiasha ku kuwawezesha Vijana hawa kujenga ajira kwa vijana wengine huku wakichochea upatikanaji wa bidhaa na huduma katika jamii inayowazunguka.

Kufuatia hatua hiyo baadhi ya wajasiriamali waliohudhuria warsha hiyo wameishukuru Airtel kwa mchakato huo na wameiomba Airtel kuendelea na zoezi hilo kwa wafanyabishara nchi nzima ili waweze kufahamu umuhimu wa kufanya biashara kwa malengo zaidi.

Aisha Mtangi ni mfanyabiashara mdogo anayejihusisha na biashara ya kuuza matunda aliyenufaika na mafunzo hayo ambaye alisema, “kuwa kwa sasa amepata muongozo mzuri utakaokuza biashara zake na kuzifanya kwa weledi mkubwa zaidi”

“Hii ni fursa ya kipekee kwangu kama kijana na ninaishukuru sana Airtel kwa mafunzo yenye manufaa kwangu na vijana wenzangu wa hapa Tanga” Alisema Aisha.

Airtel imejipanga kufikia mikoa 10 kote Tanzania hadi kufikia December mwaka huu. Vijana wa mikoa hii watanufaika na mafunzo ya Ujasiriamali na vitendeakazi kwaajili ya kukuza biashara zao.

Leave A Reply