Ali kiba alivyomwangushia mwanaye pati
Stori: Hamida Hassan
Eee Bwana Dah! Mwanamuziki Ali Kiba pamoja na ubize wake juzikati alionesha jinsi alivyo karibu na watoto wake baada ya kumuangushia bonge la pati mwanaye Amaya ikiwa ni siku yake ya kuzaliwa.
Pati hiyo ilihudhuriwa na ndugu wa karibu wa staa huyo akiwemo bibi wa mtoto huyo (mama wa Kiba) huku watu wakimpongeza Kiba kwa jinsi anavyojitahidi kuonesha upendo kwa wanaye.
“Dah! Jamaa humwambii kitu kwa wanaye, anawapenda sana,” alisema shabiki wake aliyehudhuria pati hiyo.