The House of Favourite Newspapers

Amuua Kaka Yake Kisa Makalio ya Mwanamke

0
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaizidizi Jonathan Shanna Warioba, ametoa onyo kali kwa wananchi wenye tabia za udhalilishaji kwa wanawake kuacha tabia hiyo mara moja huku akisema kwamba udhalilishaji umesababisha kifo.
Kamanda Shanna amelazimika kusema hayo wakati akitolea ufafanuzi juu ya tukio la mauaji ya mkazi wa Kijiji cha Vilabwa Wilaya ya Kisarawe Imma Habibu (26).
Kwa mujibu wa Shanna Marehemu aliuwawa juzi majira ya saa mbili asubuhi wakati walipokuwa kijiweni na wenzake baada ya kutokea ugomvi kati yake na Ramadhani Habibu (23) ambaye ni ndugu yake, baada ya mwanamke mmoja ambaye anadaiwa kuwa na maumbile makubwa (makalio) kupita, mbele yao.
Alisema baada ya mwanamke huyo kupita mbele yao walianza mabishano ambapo marehemu alisema mwanamke huyo ana makalio makubwa na Ramadhani alisema ni makalio ya kawaida sio  makubwa.
Kamanda Shanna alieleza kuwa baada ya mabishano hayo ndipo ulipozuka ugomvi hadi kufikia hatua ya Ramadhani kumchoma kisu kaka yake kifuani, upande wa kulia na alifariki dunia akiwa njiani anapelekwa hosptali ya kisarawe.
Alisema jeshi la polisi linamshikilia mtuhumiwa kwa kufanya mauaji hayo na kuwa atafikishwa mahakamani mara moja  na kuwa amekubali kuwa amefanya mauaji hayo.
Kufuatia,tukio hilo Kamanda Shanna aliendelea kutoa onyo kwa wananchi na  vijana wanaoshinda vijiweni kuacha tabia ya udhalilishaji hasa kwa wanawake na kuwa  kufanya hivyo ni kosa kisheria na kuwa kama kuna mtu aliyefanyiwa vitendo vya namna hiyo atoe taarifa polisi na atafikishwa mahakamani.
“Wito kwa wale wanaokiuka haki za binadamu kwa kumdhalilisha mtu waache mara moja, mfano kisheria hata kumkonyeza mtu ni kosa la jinai hivyo unapaswa kufika polisi, na tutamfuatilia kisha kumpeleka mahakamani” Kamanda Shana amefafanua
Pia kamanda Shanna ametoa rai kwa wanawake kuvaa nguo zinazositiri maungo yao ili kuepusha vishawishi na matamanio kwa wanaume
Leave A Reply