The House of Favourite Newspapers

Carlo Ancelotti Atimuliwa Bayern Munich

0

Kocha wa Bayern Munich, Carlo Ancelotti amefutwa kazi jana kufuatia mwanzo mgumu wa msimu wa 2017/18 yakiwemo matokeo ya juzi usiku ambapo timu hiyo ilikubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa PSG anayoichezea Neymar Jr.

Mkurugenzi mtendaji wa Bayern Munich Karl-Heinz Rumminigge alionekana kuchukizwa na matokeo ambapo alisema Bodi ya timu itakuwa na kikao na kocha Ancelotti mchana wa leo baada ya timu kurejea kutoka Paris Ufaransa.

Mchana huu Sky Sports imethibitisha kuwa baada ya kikao Bodi imefikia maamuzi ya kusitisha kibarua cha kocha huyo raia wa Italia.

Ancelotti mwenye miaka 58 ameitumikia Bayern kwa msimu mmoja wa 2016/17 baada ya kuchukua nafasi ya Pep Gaurdiola ambaye alijiunga na Manchester City. Muitaliano huyo ameiwezesha Bayern kutwaa ubingwa wa Bundesliga msimu uliopita.

Leave A Reply