The House of Favourite Newspapers

Aussems: Naiona Simba Fainali ya Caf

0

WAKATI droo ya Hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikitarajia kupangwa leo Ijumaa, kocha wa zamani wa Simba, Mbelgiji, Patrick Aussems ameibuka na kusema kuwa timu hiyo ina nafasi kubwa ya kuweza kufika fainali katika michuano hiyo kutokana na kurekebisha mambo mengi aliyoshauri wakati yupo ndani ya timu hiyo.

 

Aussems ambaye kwa sasa ni kocha wa AFC Leopards ya Kenya licha ya kuwa kwenye mapumziko nchini Ufaransa baada ya Ligi ya Kenya kusimama kutokana na kuwepo kwa ‘lockdown’ ya Corona, aliondoka Simba mwaka 2019 baada ya kutimuliwa kutokana na mwenendo mbaya wa timu.

Aussems ameliambia gazeti hili kuwa Simba ya sasa imebadilika kutokana na kukamilisha miondombinu yake, hivyo inaweza kufanya chochote tofauti na wakati wake alipokuwa kwenye timu hiyo.

 

“Unajua wakati ule Simba hakuwa na miondombinu mizuri wala uwanja wake wa mazoezi kwa sababu tulikuwa tufanya mazoezi katika viwanja vya watu wakati mwingine Uwanja wa Boko na wakati mwingine Uhuru tena ikiwa ni kwa kusubiri wenye timu zao wamalize kwanza.

 

“Lakini sasa Simba inamiliki kila kitu kama zilivyo timu nyingine kubwa Afrika ndiyo maana inaweza kufanya vyema katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na ubora ambao inaonyesha naona wanayo nafasi kubwa ya kucheza fainali kwa kuwa ni timu ambayo imepiga hatua kubwa,” alisema Aussems.

Stori: Ibrahim Mussa,Dar es Salaam

Leave A Reply