Beki Kisiki Daniel Amoah Asaini Mkataba Mpya Azam FC
BEKI kisiki wa Azam FC, Daniel Amoah, amesaini nyongeza ya mkataba mpya wa mwaka mmoja zaidi kuendelea kusalia kwenye viunga vya Azam Complex.
Mkataba wa awali wa Amoah ulikuwa ufikie ukomo Agosti 2024 lakini sasa mkataba huo utamfanya aendelee kuwatumikia Waoka Mikate hao mpaka mwaka 2025.
Amoah (25) raia wa Ghana amekuwa na kiwango kizuri katika eneo la ulinzi la Wanalambalamba hao tangu ajiunge na nao mnamo Agosti, 2016 akitokea Medeama ya nchini kwao.