The House of Favourite Newspapers

Brazil: Watu 2,286 Wafariki kwa Covid19 ndani ya Saa 24

0

Siku ya Jumatano watu 2286 wameripotiwa kufariki dunia kutokana na Ugonjwa wa Corona nchini #Brazil kwa mujibu wa takwimu za Chuo Kikuu cha Hopkins kilichopo Marekani.

 

 

Brazil ambayo ni nchi ya pili kwa kuathiriwa na #CoronaVirus imerekodi jumla ya vifo 268,370 tangu virusi viingie nchini humo.

 

 

Wataalamu wa Afya wameonya kutokana na kuzidiwa kwa Miundombinu ya Afya nchini humo huku virusi vipya vya Corona vikionekana kuwa na nguvu kubwa.

 

Rais wa Brazil analaumiwa kwa kuonesha uzembe kudhibiti maambukizi ya Virusi vya Corona huku Rais wa zamani wa nchi hiyo, Luis Inacio Lula da Silva amewataka Wananchi kupatiwa chanjo

Leave A Reply