JPM Amkabidhi Simbachawene Mikoba ya Lugola, Zungu Aula – Video
Rais Dkt. John Magufuli leo Januari 23, 2020 amemteuwa Mbunge wa Ilala Dar es salaam, Mussa Azzan Zungu kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.
Rais pia amemteuwa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, George Simbachawene kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Simbachawene anachukua nafasi ya Kangi Lugola, ambaye uteuzi wake umetenguliwa leo Januari 23, 2020 na Rais Magufuli kwa kile alichoeleza kutoridhishwa na utendaji kazi katika Wizara hiyo.
Aidha Rais Magufuli amemteua Meja Jenerali Jacob Kingu kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi leo Jenerali Kingu alikuwa Katibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani mpaka jana Januari 22,2020 ambapo aliandika barua ya kujuizulu nafasi hiyo na Rais akakubali ombi lake.
Rais Magufuli amefanya uteuzi wa mabalozi watatu, Meja Jenerali Jacob Kingu, Kamishina Jenerali wa Magereza Faustine Kasike na Dkt.John Steven Simbachawene ambao vituo vyao vya kazi vitatangazwa baadaye.