Breaking News: Samatta Mchezaji Bora Afrika 2015
Mshambuliaji Mbwana Ally Samatta wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe ameshinda Tuzo ya Mchezaji bora anayecheza soka barani Afrika na kuwamwaga Baghdad Boundjah (Algeria/: Etoile du Sahel) na Robert Kidiaba (DR Congo/ TP Mazembe) Usiku huu mjini Abuja, Nigeria.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta (kushoto) akiwa mshambuliajinwa Gabon, Pierre-Emerick Emiliano François Aubameyang katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa mjini Abuja, Nigeria usiku huu wakati hafla ya Tuzo za Wachezaji Bora wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mwaka 2015.
Hongera kabisa unastaili kupata tuzo isikuleweshe ukasahau ku endelea mazowezi na mwaka 2017 liwe lako. Belgium nayijua sana ukindelea kufanya vizuri ni njia muhimu kuingia Premier league na kujipatia mshahara wa kutisha. Hongera sana tena
Ushindi wako Samatta ni sifa kubwa kwako, kwa klabu yako na kwa TANZANIA. Pamoja na kulitangaza jina lako, umeitangaza pia TANZANIA kimataifa! Kila la heri na asante kwa kututangaza sote.
ni shangw saana twajivunia km watanzania kutangazw kw bwana ally samatta kuw mchezaj bora afrika ni jambo zuli namtakia hongera na nafanikio mazuli aliyo yaonyesha kikubw asijisahau akaze buti zaid ya hapo
Hongera sana Mbwana Samatta kwa hatua kubwa hiyo uliyoifikia na kulitangaza jina lako, timu yako na taifa letu Tanzania katika medali ya soka. Mungu akutangulie uweze kutimiza ndoto zako za kusakata kandanda ulaya. Nawaomba na wachezaji wengine wazawa waige mfano wa Samatta wasibweteke wakaze butu, nidhamu na kujituma katika soka watafanilkiwa.
Hongera sana..
Sports Marking on World Map!
Congrats Mbwana Sammata.