Caf Yambana Matola, Atakiwa Kusoma
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetoa mwongozo kwa klabu zitakazoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho msimu ujao kuwa kocha Mkuu LAZIMA awe na Leseni A na Msaidizi wake B.
Hii inamaanisha kuwa kocha msaidizi wa Simba, Selemani Matola mwenye Leseni C ya CAF hataruhusiwa kukaa kwenye benchi mpaka atakapohitimu mafunzo ya Leseni B.