Caroline: Siwezi kuacha kuwaka
MASTAA wengi kunako kiwanda cha filamu Nollywood imekuwa jambo la kawaida kuwakuta wakiwa katika ngozi ambayo hawakuwa nayo zamani (kujichubua).
Caroline Danjuma ni mmoja kati ya mastaa hao ambaye ngozi yake imekuwa tofauti na ilivyokuwa awali ambapo alikuwa mweusi lakini kwa sasa ni mweupe.
Kupitia Instagram yake, Caroline anayejulikana zaidi kupitia filamu ya Stalker alinangwa na mashabiki wake juu ya ngozi yake kuwa nyeupe kupitiliza huku wengi wakimtaka arudi kama zamani ambapo aliwajibu;
“Siwezi kuacha kuwaka. Rangi hii ya dhahabu imebadilika tu sikuzaliwa hivi nammis kuwa kama zamani.”