Combination ya Dk Shika na Ebitoke Usiku wa 900 ITAPENDEZA (Video)
WAKAZI wote wa jiji la Dar es Salaam, wametakiwa kukaa tayari na kujiandaa kwa Tamasha kubwa litakalofanyika usiku wa Desemba 9, 2017, katika ukumbi wa Taifa wa Burudani Dar Live, ambalo ni maalum kwa ajili ya Dkt Louis Shika, ambaye amejipatia umaarufu mkubwa kupitia nyumba za Mfanyabiashara, Said Lugumi, alizotaka kuzinunua.
Tamasha hilo la kipekee kwa Dkt Shika, litahusisha pia baadhi ya wasanii akiwemo Wachekeshaji, Ebitoke na Maufundi, pamoja na wasanii wa muziki wakiwemo, Linex, Prince Amigo na Bendi ya Twanga Pepeta.
Comments are closed.