DC JOKATE ATUA +255 GLOBAL RADIO, AIMWAGIA SIFA
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo amefanya ziara katika Ofisi za Makampuni ya Global Group na kutoa pongezi za dhati kwa namna ilivyompa supoti katika kazi zake mbalimbali.
Pia, DC Jokate amefurahishwa kwa kuanzishwa radio ya +255 Global Radio ikiwa na lengo la kumfikia kijana kisasa zaidi. Mkuu huyo wa wilaya alizungumzia pia mradi wa kuendeleza elimu wilayani kwake aliouita Tokomeza Ziro ambapo Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani atakuwa mgeni rasmi Machi 30 mwaka huu katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar.
Kusikiliza +255 Global Radio => LISTEN LIVE
PICHA NA MUSA MATEJA | GPL
Comments are closed.