The House of Favourite Newspapers

Rais wa Zamani Marekani Donald Trump Ashtakiwa kwa Ubakaji New York

0

Mwandishi E Jean Carroll amemshtaki Donald Trump katika jimbo la New York Marekani kwa madai ya kumbaka katika miaka ya 1990.

 

Bi Carroll ni miongoni mwa wa kwanza kushtaki chini ya Sheria ya Watu Wazima Walionusurika, ambayo ilianza kutekelezwa siku ya Alhamisi.

 

Sheria ya serikali inaruhusu muda wa mwaka mmoja kwa waathiriwa kuwasilisha kesi za unyanyasaji wa kijinsia huko New York kwa madai ambayo yangevuka mipaka ya sheria.

 

Rais huyo wa zamani amekanusha madai dhidi yake.

Bi Carroll anadai kuwa shambulio hilo lilitokea katika chumba cha kuvaa cha duka la kifahari la New York miaka 27 iliyopita.

 

Sheria ya Waathirika wa Watu Wazima inaruhusu waathiriwa kujitokeza ikiwa unyanyasaji wa kijinsia ulitokea walipokuwa na umri wa zaidi ya miaka 18.

 

Bi Carroll pia amemshtaki Rais wa zamani Trump kwa kumharibia jina baada ya kumshutumu kwa kusema uwongo alipotangaza hadharani madai yake kwa mara ya kwanza mwaka wa 2019. Bw Trump ameyataja madai ya Bi Carroll kuwa “ya kubuni”.

 

Kesi ya madai ya kesi hiyo imepangwa kusikizwa tarehe 6 Februari.

Katika taarifa, wakili wa Bi Carroll, Roberta Kaplan, alisema kesi mpya iliyowasilishwa Alhamisi inanuiwa kumwajibisha Bw Trump kwa madai ya kushambuliwa.

KOMBE LA DUNIA QATAR: TIMU ZA KIAFRIKA HALI TETE, MATUMAINI YAZIDI KUWA MAGUMU…

Leave A Reply