Erasto Nyoni Kukipiga Namungo Msimu Ujao
Baada ya Wekundu wa Msimbazi Simba kumpa mkono wa kwaheri mchezaji wao Erasto Nyoni hapo jana, Mapema hii leo Nyoni ametangazwa na Namungo kutoka Lindi kwamba atakipiga katika timu hiyo kwa msimu ujao.
Kupitia ukurasa wao wa Instagram Namungo wameandika “Tunayofuraha kuwataarifu kuwa Erasto Edward Nyoni amejiunga kuitumikia Timu yetu ya Namungo Fc akitokea Simba Sc.
Karibu kwenye Familia ya Wauwaji wa Kusini Erasto Edward Nyoni #southenkillers”