The House of Favourite Newspapers

ESHA: JOKATE USINICHUKIE KISA KIBA

Esha Buheti.

ESHA Buheti amefunguka kuwa kama mwanamitindo maarufu Jokate Mwegelo, anamchukia kisa mwanamuziki Ali Saleh Kiba ‘AliKiba’ kuoa, atakuwa anamkosea sana.

Akipiga stori na Over Ze Weekend, Esha ambaye amefanya poa kwenye filamu ya Jini Aulat, alisema kuwa ames-ikia kutoka kwa watu wake wa karibu kwamba mwanamitindo huyo anamchukia kwa sasa kutokana na kuwa karibu na Kiba kwenye harusi yake na mrembo Amina Khaleef wa Kenya.

Kiba na mkewe.

Alisema mbali na hilo, pia anahisi hivyo maana tofauti na zamani Jokate alipokuwa akitazama vitu vyake mitandaoni na kumsapoti lakini siku hizi mrembo huyo hafanyi.“Kama ni kweli Jokate atakuwa ananichukia kisa mpenzi wake wa zamani Kiba kuoa kama watu wanavyosema, basi atakuwa ananichukia bure.

Jokate.

“Mimi ni kama bendera tu nafuata upepo kwa hiyo wa kumchukia ni Kiba mwenyewe aliyeamua kumuacha yeye na kuoa mtu mwingine, na wala si yeyote yule ambaye yupo karibu na Kiba,” alisema Esha.

IMELDA MTEMA

Comments are closed.