The House of Favourite Newspapers

Esma: Sishobokei mali za Diamond

0

ESMA-(1)Esma Abdulkadiri ‘Esma Platnumz’

STORI: IMELDA MTEMA, WIKIENDA

DAR ES SALAAM: Dada wa Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Abdulkadiri ‘Esma Platnumz’ amesema kuwa kamwe hawezi kushobokea mali za kaka yake huyo kwa kuwa na yeye ana uwezo wa kutafuta zake.

Akizungumza na Wikienda, Esma aliweka wazi kuwa siku zote mtu anayetumainia cha ndugu yake hufa maskini hivyo na yeye ameamua kujiingiza kwenye ujasiriamali ambao unampatia kipato.

“Wengi wanajua mimi nashobokea mali za Diamond, si kweli kwa sababu na mimi nina uwezo wa kutafuta za kwangu kwani nina biashara nzuri tu,” alisema Esma aliyezaa na Petit Man.

Leave A Reply