The House of Favourite Newspapers

Guinea: Wanajeshi Wadaiwa Kumpindua Rais Alpha Conde

0

Hatima ya Rais wa Guinea Alpha Condé haijulikani wazi baada ya video ambayo haijathibitishwa kumuonyesha mikononi mwa wanajeshi, ambao walisema wamefanya mapinduzi.

Walakini, waziri wa ulinzi amenukuliwa akisema jaribio la kuichukua serikali lilikuwa limeshindwa.

Hii inafuatia masaa mengi ya makabiliano ya risasi karibu na Ikulu ya rais katika mji mkuu, Conakry.

Wanajeshi wa Guinea wamejitokeza katika runinga ya taifa wakithibitisha kwamba rais Alpha Conde ameondolewa madarakani.

Wanajeshi hao wametangaza kuwa nchi hiyo itakuwa chini ya Serikali ya Mpito huku baadhi ya video zikimuonesha Rais Alpha Conde akiwa chini ya Maafisa wa Jeshi.

Leave A Reply