The House of Favourite Newspapers

Henry: Messi Hatoshi PSG

0

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry amesema kuwa kitendo cha PSG kumsajili Lionel Messi siyo suluhisho la matatizo yao.


PSG walimsajili Messi
wiki iliyopita na anatarajiwa kuanzia mazoezi na timu hiyo kabla ya mwisho wa wiki hii.Henry amesema pamoja na kwamba Messi ataisaidia PSG lakini hawezi kuwa suluhisho la matatizo yote kwenye timu hiyo. Mshambuliaji huyo wa zamani wa timu ya Taifa ya Ufaransa, amesema timu hiyo kwa misimu ya hivi karibuni imeruhusu mabao mengi sana na hilo lilitakiwa kuwa suluhisho la kwanza.

 

“PSG wamemsajili Lionel Messi huu ni usajili mkubwa sana, lakini ni vyema pia wakawa makini sana pia kwenye eneo la ulinzi kwa kuwa waliruhusu mabao mengi sana kwenye msimu uliopita.

“Kuhakikisha wanakuwa na kikosi kichobalansi ni jambo jema zaidi, tumekuwa tukizungumza kuhusu wachezaji bora wa eneo la ushambuliaji lakini huku nyuma napo ni sehemu muhimu sana.

 

Tunamzungumzia Messi ambaye alikuwa akiitumikia Barcelona lakini watu wanasahau kuwa PSG iliruhusu mabao mengi msimu uliopita. ‘Kwa ujumla ukiwa na timu ambayo hairuhusu mabao mengi ipo karibuni sana na ubingwa,” alisema Henry raia wa Ufaransa.

 

Messi ataungana na Kylian Mbappe pamoja na Neymar kuhakikisha wanakuwa na safu bora zaidi ya ushambuliaji.Hata hivyo, timu hiyo pia imemsajili Sergio Ramos kutoka Real Madrid.

Leave A Reply