The House of Favourite Newspapers

Hukumu Kuhusu Bomoabomoa Kutolewa Kesho

0

3.Baadhi ya wananchi walofika mahakama hapo wakiwa nje ya maduka yaliyopo nje ya mahakama hiyo. Wakili wa mlalamikaji anayesikiliza kesi hiyo, Abubakar Salim, akihojiwa na wanahabari baada ya kutoa taarifa kwa wakazi waliobomolewa nyumba zao mabondeni waliokuwa wamejitokeza kusikiliza kesi ambayo maamuzi yake yatatolewa kesho.

2.Wananchi wakimsikiliza wakili huyo juu ya kuahirishwa kwa kesi hiyo hadi hapo kesho.Wananchi wakimsikiliza wakili Salim (hayuko pichani).1.Wakili wa walalamikaji anayesikiliza kesi hiyo akihojiwa na wanahabri baada ya kuwapa taarifa wakazi waliobomolewa Nyumba zao za mabondeni kuwa kesi hiyo itasikilizwa hapo kesho.Baadhi ya wananchi waliofika mahakamani  hapo.

KESI ya kupinga bomoabomoa iliyotarajiwa kutolewa maamuzi leo jijini Dar es Salaam katika Mahakama Kuu kitengo cha ardhi imeahirishwa tena,  badala yake hukumu itatolewa kesho.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulya, (CUF) ambayo inataka wananchi hao mbali na kubomolewa wapewe maeneo mbadala na yenye usalama ambapo wakili wa upande wa mlalamikaji akiwa ni Abubakar Salim aliyewataka wananchi waliokuwa nje ya mahakama hiyo kutochoka kuendelea kufuatilia kesi hiyo.

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply