The House of Favourite Newspapers

Huu Ndiyo Mlima wa Simba CAF

0

 

MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2020/21 ambayo inaandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), inatarajiwa kuanza wikiendi hii ikiwa ni mara ya 57 tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo lakini ni mara ya 25 tangu kuanza kutumika kwa mfumo huu unaotumika sasa.

 

Bingwa wa msimu huu atapata nafasi ya kushiriki mechi ya CAF Super Cup mwakani, pia timu tatu za juu zitafuzu kucheza michuano ya Kombe la Dunia la Klabu nchini China mwakani pia.

 

Mataifa yanavyotoa timu

Wanachama wote 56 wana haki ya kupata timu shiriki katika michuano hiyo, mashirikisho na vyama vya mataifa 12 ambayo yana viwango vya juu kwa pointi za Caf walizopata ndani ya miaka mitano iliyopita, wanapewa nafasi ya kupeleka timu mbili ndani ya msimu mmoja.

Hivyo kwa mujibu wa hesabu hizo, ni wazi kuwa idadi ya timu shiriki ambazo zinatakiwa kuwemo kuanzia hatua ya awali ni 68 lakini idadi hiyo haijawahi kutimia kutokana na sababu mbalimbali.

 

Pointi za ubora huwa zinapatikana kutokana na ubora wa timu ngazi ya klabu kwa hatua zinazopitia au kufika ndani ya miaka mitano tangu msimu husika unaotakiwa kufanyika kwa michuano husika.

 

Utaratibu huu wa kuhesabu pointi pia unahusika hata katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

 

Utaratibu wa pointi za ubora upo hivi…

Ligi ya Mabingwa  Kombe la Shirikisho

Bingwa           6 pointi          5 pointi

Wa pili            5 pointi          4 pointi

Nusu Fainali  4 pointi          3 pointi

Robo Fainali 3 pointi          2 pointi

Wa 3 kundini 2 pointi          1 pointi

Wa 4 kundini 1 pointi          0.5 pointi

 

Ili kupatikana kwa pointi husika kwa taifa, sasa kinachofuata hapo ni kuwa idadi ya pointi zinazidishwa kwa idadi maalum kulingana na miaka ambayo timu zimefika hatua fulani.

Yaani ile timu ambayo au ambazo zimefika hatua ya mbali mwaka jana pointi zake zinazidishwa mara 5, zile za mwaka juzi zinazidishwa mara 4. Mfano kama Tanzania ina pointi 10 kutokana na pointi ilizopata kwa mafanikio ya klabu yake, idadi hiyo inazidishwa mara 5 au 4 au 3 kwa kutegemea na mwaka wa hatua ya mwisho waliyofika katika mwaka wao wa mwisho kushiriki katika michuano.

 

Hii inamaana kuwa utaratibu huu unakuwa unaendelea hivyohivyo, kabla ya msimu kuanza, mahesabu yanapigwa na ile ambayo imefanya vizuri ndani ya mwaka mmoja uliopita kabla ya michuano husika, inakuwa na nafasi kubwa ya kupata pointi nyingi zaidi.

 

Mfano wa utaratibu wa pointi zilivyohesabiwa kuelekea kuanza kwa msimu huu upo hivi:

2019–20: x5

2018–19: x4

2018: x3

2017: x2

2016: x1

Timu

Kutokana na janga la Ugonjwa wa COVID-19, mashirikisho na vyama mbalimbali vilisitisha ligi zao na kuamua kuchagua washiriki kwa vigezo vya waliokuwa kileleni kupewa nafasi.

Pointi za ubora wa nchi shiriki

Kuelekea kuanza kwa msimu huu, inamaanisha kuwa mahesabu ya pointi zilipigwa kulingana na ushiriki wa timu kuanzia mwaka 2016 hadi 2020 katika michuano hiyo inayosimamiwa na CAF:

 

Wanaoingiza timu mbili msimu huu kutokana na pointi zao:

 

Nchi   Pointi      Timu shiriki

  1. Morocco 190 Raja Casablanca, Wydad Casablanca
  2. Misri 167 Al Ahly, Zamalek
  3. Tunisia 140 Espérance de Tunis, CS Sfaxien
  4. DR Congo 83 TP Mazembe, AS Vita Club
  5. Algeria 81 CR Belouizdad, MC Alger
  6. Afrika Kusini 68.5 Mamelodi Sundowns, Kaizer Chiefs
  7. Zambia 43 Nkana, Forest Rangers
  8. Nigeria 39 Plateau United, Enyimba
  9. Guinea 38 Horoya, Ashanti de Siguiri
  10. Angola 36 Petro de Luanda, 1º de Agosto
  11. Sudan 29.5 Al Merrikh, Al Hilal
  12. Libya 16.5 Al Nasr, Al Ahly Benghazi

 

Wanaoingiza timu moja msimu huu kutokana na pointi zao:

Nchi    Pointi    Timu shiriki

  1. Tanzania 14 Simba
  2. Ivory Coast 13 RC Abidjan
  3. Kenya 11 Gor Mahia
  4. Zimbabwe 11 FC Platinum
  5. Msumbiji 9 Costa do Sol
  6. Congo 8 AS Otohô
  7. Uganda 8 Vipers
  8. Ghana 6.5 Asante Kotoko
  9. Mali 6.5         Stade Malien
  10. Rwanda 6 APR
  11. Eswatini 5 Young Buffaloes
  12. Ethiopia 4 Mekelle 70 Enderta
  13. Botswana 3 Jwaneng Galaxy
  14. Togo 3 ASKO Kara
  15. Benin 2.5 Buffles du Borgou
  16. Mauritania 2.5 FC Nouadhibou
  17. Burkina Faso 2 Rahimo
  18. Cameroon 2 PWD Bamenda
  19. Gabon 1 AS Bouenguidi

 

Burundi          —            Le Messager Ngozi

Chad               —            Gazelle

Comoros        —            US Zilimadjou

Djibouti         —            GR/SIAF

Equatorial Guinea     —            Akonangui

Gambia         —            Gambia Armed Forces

Lesotho         —            Bantu

Niger             —            AS SONIDEP

Senegal         —       Teungueth

Somalia         —      Mogadishu City

Zanzibar         —        Mlandege

 

 

Mataifa ambayo hayajaingiza timu msimu huu:

Cape Verde Central African Republic Eritrea Guinea-Bissau Liberia Madagascar Malawi Mauritius Namibia Réunion São Tomé and Príncipe Seychelles Sierra Leone South Sudan.

 

Ratiba

Michuano imechelewa kuanza sababu kubwa ilikuwa maambukizi ya Covid-19. Mechi za kwanza zitachezwa Novembea 27-29, marudio ni Desemba 4-6, mwaka huu.

 

Raundi ya Awali

Nov 27-29 & Des 4-6

 

Raundi ya Kwanza

Des 22-23 & Jan 5-6

 

Hatua ya Makundi

Februari         12-13, 2021

Februari         23-24, 2021

Machi     5-6, 2021

Machi             16-17, 2021

Aprili               2-4, 2021

Aprili               9-11, 2021

 

Robo fainali

Mei 14-16 &  Mei 21-23

 

Nusu Fainali

Juni 18-20 & Juni 25-27

Fainali

Julai 17, 2021

Raundi ya Awali ipo hivi…

Kutakuwa na mechi mbili, nyumbani na ugenini, timu zikilingana pointi na mabao, faida ya bao la ugenini itatumika, hapo napo wakilingana watapigiana penalti, hakutakuwa na dakika 30 za nyongeza, lakini wikiendi hii mambo ni hivi:

 

Ashanti de Siguiri   v   Stade Malien, Gambia Armed   v     Teungueth  RC Abidjan            v      ASKO Kara

AS SONIDEP          v      Mogadishu City

Al Ahly Benghazi  v      Mekelle 70 Enderta

Gazelle           v      GR/SIAF

Forest Rangers     v      AS Bouenguidi

Jwaneng Galaxy   v      US Zilimadjou

Young Buffaloes   v      Le Messager Ngozi

PWD Bamenda     v      Kaizer Chiefs

AS Otohô               v      Al Merrikh

Rahimo          v      Enyimba

FC Nouadhibou    v      Asante Kotoko

Vipers                     v      Al Hilal

Buffles            v      MC Alger

Mlandege              v      CS Sfaxien

Bantu             v      Nkana

Akonangui             v      Petro de Luanda

Costa do Sol v      FC Platinum

Plateau United     v      Simba

CR Belouizdad      v      Al Nasr

APR                         v      Gor Mahia

 

Raundi ya Kwanza

Timu 10 zimeshawekwa katika kundi hili kusubiri zile za Raundi ya Awali, hii ni kutokana na ubora wao waliouonyesha ndani ya miaka mitano iliyopita. Hivyo zitakutana na zile

 

Ashanti /Malien           v      Wydad Casablanca

Armed/Teungueth       v      Raja Casablanca

RC Abidjan/ASKO                 v      Horoya

SONIDEP/Mogadishu v      Al Ahly

Al Ahly/Mekelle           v      Espérance de Tunis

Gazelle/GR                    v      Zamalek

Forest/Bouenguidi               v      TP Mazembe

Galaxy/Zilimadjou               v      Mamelodi

Buffaloes/Ngozi           v      AS Vita Club

PWD/Kaizer Chiefs              v      1º de Agosto

Otohô /Merrikh            v      Rahimo/Enyimba

Nouadhibou/Kotoko   v      Vipers/Al Hilal

Buffles/MC Alger         v      Mlandege/Sfaxien

Bantu/Nkana        v      Akonangui/ Luanda

Costa/Platinum            v      Plateau/Simba

CR Belouizdad/Al Nasr        v      APR/Gor Mahia

Na John Joseph

 

Leave A Reply