The House of Favourite Newspapers

Ishu ya Mtoto Bado Inamtesa Wema!

0

DAR: Bado ishu ya kutopata mtoto inamtesa kinoma staa wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu. Wema ameonesha kukerwa na kuchukizwa na wale wanaotonesha kidonda chake cha kutopata mtoto kwenye mitandao ya kijamii.

 

Akizungumza na Gazeti la IJUMAA kuhusu ishu hiyo, Wema kuwa, watu waache kumkejeli kwani yeye si mwanamke wa kwanza kukosa mtoto.

 

“Najua sitakuwa mwanamke wa kwanza kukosa mtoto.

“Mimi naridhika tu na kitendo cha kuwapenda watoto hata kama sina wa kwangu.

“Yote ni mipango ya Allah, mimi ni mja wake tu, ila siyo kwamba sitaki, namtamani sana, lakini siyo maajaliwa yangu basi.

 

“Mimi nawashauri watu wasipende kuzungumza vitu vinavyoumiza wenzao kwa sababu kiukweli hata mimi sipendi hivyo,” amesema Wema mwenye umri wa miaka 31 ambaye kwa muda mrefu amekuwa akieleza matamanio yake ya kupata mtoto huku akiumizwa na watu wanaomuita mgumba.

Stori: Imelda Mtema. Ijumaa

Leave A Reply