The House of Favourite Newspapers

Ishu ya Onyango Kwenda Orlando Pirates Ipo Hivi

0

MLINZI wa kati wa klabu ya Simba, Mkenya, Joash Archieng Onyango almaarufu ‘Chuma’ amesema kwasasa bado hajapata taarifa yeyote kuhusu yeye kuhitajika na klabu ya Orlando Pirate ya nchini Afrika Kusini.

 

Joash Onyango amesema; “Bado sijapata taarifa zozote kuhsu hilo.”

 

Tokea ajiunge na kikosi cha Simba mwanzoni mwa msimu huu, Onyango ameoneha kiwango bora na kuwa mlinzi chaguo la kwanza tegemeo kikosini na kuzidi kuvivutia vilabu vikubwa barani Afrika mpaka kuhusishwa na klabu ya Orlando Pirates.

 

Onyango amefunga bao moja kwenye ligi kuu bara tena likiwa ni la kuisawazishia Simba kwenye mchezo dhidi ya Yanga na kuufanya mchezo uishe kwa sare ya bao 1-1 na kutengeneza nafasi moja ya bao kwa kumpasia John Bocco aliyefunga bao pekee dhidi ya klabu ya Mwadui.

Leave A Reply