Izzo B aanika undugu wake na Master J
Na BONIPHACE NGUMIJE
MSANII wa Hip Hop Bongo anayeunda Kundi la The Amaizing, Emmanuel Simwenga ‘Izzo B’ amefunguka kuwa ushikaji wake na mkali wa midundo anayemiliki studio ya Mj Records, Joachim Kimaryo ‘Master J’ ulishapitiliza na kuwa undugu.
Akistorisha na safu hii iliyokaa kiburudani, Izzo B alisema kuwa, ameanza kupiga kazi na Master J kuanzia mwaka 2009 na ni yeye aliyempokea jijini Dar akitoka kwao Mbeya kwa ajili ya ‘kuhuso’ kimuziki.
“Ninamheshimu sana Master J, ni mtu wangu wa karibu ambaye naweza kusema ushikaji wetu ulishafika mbali na kuwa undugu maana tunasaidiana kwenye mambo mengi mno, ndani na nje ya kazi,” alisema Izzo.