Jengua Azikwa Makaburi ya Mburahati Dar Leo (Picha +Video)
MASTAA, ndugu na jamaa leo wameungana kuuzika mwili wa aliyekuwa mwigizaji wa filamu za Kibongo, Mohamed Fungafunga, maarufu kama Jengua.
Jengua alifariki jana nyumbani kwa mwanaye, Mkuranga mkoani Pwani alipokuwa akipatiwa matibabu na kuzikwa leo mchana makaburi ya Mburahati Jijini Dar.
Enzi za uhai wake marehemu alijipatia umaarufu mkubwa kutokana na kuigiza vizuri uhusika wa ukatili na kupenda kutamani kutoka kimapenzi na wasichana wenye umri mdogo.
Katika mazishi hayo walifurika wasanii wa tasnia mbalimbali kama vile wanamuziki, waigizaji, wanasoka, mabondia na wengineo.
HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL