The House of Favourite Newspapers

Jini Mauti-25

0

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

“Karibu mrembo,” alinikaribisha na kutulia kitini.

 

Tukaanza kuongea, kila sentensi moja aliyoizungumza ilikuwa ni lazima kuniambia kwamba alikuwa akinipenda sana. Nilibaki nikimwangalia usoni. Si kwamba sikumpenda, nilimpenda mno lakini kitu ambacho sikukitaka kabisa ni kufanya naye mapenzi tu.

Alijitahidi kuniambia maneno mengi ya kunishawishi lakini wapi, sikukubaliana naye kabisa. Alichokifanya akanisogelea, kwa sababu giza lilianza kuingia, akanishika kiuno.

Hapo ndipo aliponichanganya, ni kama aliijua sehemu hiyo ndiyo iliyokuwa ikinipa mzuka, hapohapo nikatoa mguno mmoja, akaligundua hilo hivyo kuendelea kunishika kiuno.

Ndani ya dakika kumi nilikuwa hoi, akausogeza mdomo wake na kunipumulia, pumzi yenye joto fulani ikanipiga shingoni, ikanichanganya, akaninyanyua na kwenda kwenye gesti iliyokuwa karibu na baa hiyo, tulipofika huko, akachukua chumba.

“Hemedi,” nilimuita, tayari alinitupia kitandani, nilikuwa hoi.

“Unasemaje mpenzi?” aliniuliza huku mkono wake ukiendelea kuwa kiunoni mwangu, alizidi kunipagawisha.

“Unataka tufanye nini?”

“Mpenzi yaani unakuwa hauelewi? Kwani gesti kazi yake nini?”

“Unakumbuka nilik…ahhaa…ooiishiii…” nilimwambia lakini nikashindwa kumalizia sentensi, nikaishia kuguna.

Ndani ya dakika kadhaa, wote tulikuwa kama tulivyozaliwa. Nilikuwa nahema kwa kasi, Hemedi alionekana kuwa na haraka mno, kila kitu alichokifanya alikifanya huku akiwa na presha.

Hapo ndipo nilipopata kumbukumbu juu ya kile alichokuwa akitaka kukifanya Hemedi kilikuwa cha hatari sana kwa maisha yake. Kama mtu niliyeshtuka kutoka katika jambo fulani, nikamwangalia usoni tena kwa kumkazia macho, yeye mwenyewe alinishangaa.

“Hemedi, utakufa….” nilimwambia huku nikijaribu kumsukuma.

“Nipo tayari kufa…nipo tayari kufa,” aliniambia, hakuonekana kuwa tayari kuniacha kwa siku hiyo.

Kutokana na kuwa na nguvu, nikashindwa kumsukuma, tayari alikuwa juu yangu na  alianza kufanya mchezo ule ambao sikutaka kufanyiwa na mwanaume yeyote yule. Moyo wangu uliumia mno, nilijua kile ambacho kingekwenda kutokea, nilijua kwamba Hemedi angeweza kufa kama ilivyokuwa kwa Thomas na Mudi.

Kile nilichokifikiria ndicho kilichotokea, tukaanza kufanya mapenzi, baada ya dakika moja huku akiwa juu yangu, palepale, nikaanza kuyaona macho ya Hemedi yakianza kubadilika, yakawa mekundu kama yaliyojaa damu. Akaanza kutetemeka na kutoa miguno iliyoashiria aliumia.

Akatoka juu ya mwili wangu, mapovu yakaanza kumtoka mdomoni huku damu zikitoka katika sehemu zilizokuwa wazi, puani na masikioni. Nilipoona hivyo, niliogopa mno, sikuamini kama Hemedi alikuwa akienda kufa kama ilivyokuwa kwa Thomas na Mudi.

“Aagghh….” alilia kwa maumivu makali pale chini alipokuwa.

Macho yake yakaanza kubadilika, yakatoka katika wekundu mithili ya damu na kuwa meupe kabisa, ulimi ulijigongagonga kwenye meno, kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika mwili wake, kiliniogopesha.

Nilishindwa kumsaidia kabisa, nikabaki nikimwangalia huku nikivaa haraka. Nilipomaliza, sikutaka kupoteza muda, nikaondoka kurudi nyumbani, tena huku nikikimbia.

Kifo cha Hemedi kilinitisha mno achilia mbali kuniumiza, nikawa najiuliza kwa nini hakunielewa nilipomkataza na kumweleza angefariki dunia.

“Wewe dada!” aliita msichana wa mapokezi, aliniita baada ya kuniona nikikimbia.

Itaendelea wiki ijayo.

Leave A Reply