The House of Favourite Newspapers

JK, VIONGOZI MBALIMBALI WAMFARIJI MZEE KINGUNGE

Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru ukiwasili nyumbani.
Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru, Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru ukiwasili nyumbani tayari kwa ibada maalum ya maombolezo, iliyofanyika jioni ya jana. Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es salaam.
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akimfariji Mzee Kingunge Ngomale Mwiru kwa kufiwa na Mkewe, Mama Peras Ngombale Mwiru, alipofika Nyumbani kwale Victoria, jijini Dar es salaam jana. Katikati ni Mzee Ally Mtopa.
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe wakati walipokutana kwenye Msiba wa Mama Peras Ngombale Mwiru, Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru, nyumbani kwake Victoria, jijini Dar es salaam jana.
Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba akimfariji Mzee Kingunge Ngomale Mwiru kwa kufiwa na Mkewe, Mama Peras Ngombale Mwiru, alipofika Nyumbani kwale Victoria, jijini Dar.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo akiwa ameambatana na viongozi Wengine wa Chama hicho waliofika nyumbani wa Mzee Kingunge Ngomale Mwiru kumfariji kwa kufiwa na Mkewe, Mama Peras Ngombale Mwiru.
Viongozi mbalimbali wakiongea na Mzee Kingunge.
Sehemu ya wanafamilia wakiwa ni nwenye majonzi kwa kuondokewa na mpendwa wao.
 
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete na V wamefika nyumbani kwa Mzee Kingunge Ngomale Mwiru, nyumbani kwake Victoria, jijini Dar es salaam kumfariji jana  baada ya kufiwa na mke wake Peras Ngombale hivi karibuni  na anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es.
PICHA NA MICHUZI

Comments are closed.