The House of Favourite Newspapers

 Jogoo hata akizeeka, kelele palepale!

NASHANGA! Unaringa kisa umekuja mjini kwa treni? Je, ungekuja kwa basi au ndege, si ndo ungetupanda hadi kichwani kwa miguu! Hee heeeiyaaaaa! Shoga siku zote boga ni boga tu hata liwe kubwa vipi haliwezi kuwa tikiti, upo? Nimerudi tena kama moto wa tipa usiozimwa na magari ya zimamoto yenye tenki la ujazo la maji ya kuoga, pengine utoke bafuni na sabuni mwilini. Moto wangu lazima bahari ikauke ndipo ufanikiwe kuuzima.

Huwa najiuliza; kuwafuata watoto wasiojua mapenzi, mnafuata nini au udogo wa pochi ndani inabeba mamilioni? Basi nataka kuwaeleza siku zote kama kweli una hamu na samaki, kula wa mfupa, wa miba haishi hamu. Najua ushaanza kutoa macho kama kipofu aliyebahatika kuona siku moja kwa bahati mbaya.

Nina maana gani? Nasema na wewe baba mwenye tumbo kama mkoba wa kinyozi wa chini ya mwembe. Raha ya ugomvi mpigane, hata ukipata ushindi upate wa halali na utamu wa ngoma nzuri muicheze wote. Siyo mmoja anacheza huku mwingine katulia kama ananyolewa.

Utalikuta libaba lizima jasho linamtoka kwa kupiga ngoma huku likiimba na kucheza lenyewe, mwenzake katulia akisubiri amwage mzigo wake, ampe chake ili awahi nyumbani. Kwa penzi kama hilo ni sawa na kula samaki wa miba ambaye kila ukimla haishi hamu, utaondoka na hamu zako.

Lakini ukimpata mtu mzima mwenzio, mwenye kujua mchezo, hivi jamani hamjasikia sifa ya mkoa wa Tanga au Kusini jinsi mwanaume anavyofanyiwa na mwanamke mpaka kusahau nyumbani kwake? Hii ndiyo falsafa ya mapenzi, kumkata mwenzako kiu kwa maneno na vitendo.

Sasa upo na mtoto mdogo sawa na mwanao hajui karibu mpenzi, hajui kulegeza macho, hajui sehemu gani unahitaji msaada wake, hajui kukupa maneno matamu yatakayokufanya uione safari fupi. Hajui kukupa pole baada ya safari ndefu zaidi ya asante baada ya kumpa chake.

Shoga wanakwambia jogoo hata akizeeka, sauti yake haibadiliki kamwe! Ataendelea kupiga kelele palepale na ndiyo maana raha ya mapenzi umkute mwanamke anayejua kuutumia mwili, sauti na macho yake. Mmh mashalaaaa wee acha tu ulikuwa wa kumpa elfu kumi unampa hamsini, si kwa kukuomba bali kuona alichokifanya ni zaidi ya kile utachompa.

Kufanya mapenzi na watoto wadogo ni ufataki usio na msingi zaidi ya tamaa zako wala si kufuata penzi litakalokutoa jasho hata ukiwa nyumbani ulikumbuke. Chakula kitamu ni kile kilichoungwa kikaungika na siyo kile cha kuchemsha, upo nyonyo?

Yangu ni hayo japo unaweza kusema nawaonea gere, la hasha! Mnawakomaza na kuwaharibia masomo yao kwa vizawadi uchwara vya simu na pesa, lakini huna unachokipata zaidi ya kumwaga mzigo na kuondoka.

Lakini ukitaka kukata kiu yako, nipige nikupige kutana na wataalamu kama miye Anti Nasra nikutoe kamasi. Ndiyo maana nyumba za wanawake wanaojua majukumu ya miili yao kwa waume zao, vimada hawana nafasi. Kwa leo yangu yanatosha tukutane wiki ijayo. Ni mimi Anti Nasra Shangingi Mstaafu.

Comments are closed.