Jpm Afanya Uteuzi wa RAS Simiyu
Rais Magufuli amemteua Mariam Perla Mmbaga kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu.
Kabla ya uteuzi huo, Mmbaga alikuwa Mkurugenzi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Mariam Perla Mmbaga anachukua nafasi ya Jumanne Sagini.
Mmbaga ataapishwa Jumatatu tarehe 06 Julai, 2020 saa 4:00 asubuhi Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.