JPM: Tumempoteza Mugabe Aliyekataa Ukoloni kwa Vitendo
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), John Magufuli, amemwelezea aliyekuwa rais wa Zimbabwe, hayati Robert Mugabe, kuwa alikuwa jasiri aliyeupinga ukoloni kwa vitendo.
Magufuli ameelezea hayo kupitia akaunti yake ya Twitter.
Mugabe alikuwa waziri mkuu tangu 1980 hadi 1987 alipokuwa rais mpaka anang’olewa mwaka 2017. Alizaliwa Februari 21, 1924, ambapo alitawala nchi hiyo kwa kuudhoofisha upinzani kupitia mabadiliko mbalimbali aliyoyafanya katika katiba ya nchi hiyo.
Comments are closed.