Rais Dk. John Magufuli leo Novemba 22, ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa nyumba 118 za makazi ya Askari wa Jeshi la Polisi katika eneo la Nzuguni jijini Dodoma, ambapo ujenzi huu utagharimu shilingi Bilioni 2.728 na utakamilika Desemba 31, 2019.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Magufuli amemwita na kumhiji Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, RPC Gires Muroto kuhusu pesa kiasi cha Tsh milioni tano ambazo alimpatia kwa ajili ujenzi wa Kituo cha Polisi….
RPC Muroto amesema tayari tofali 7239 mifuko ya sementi 40 na bati 65 tayari zipo na wiki kesho ataanza kwa kasi kubwa.
“Nimepita pale na kukagua mwenyewe, nimakuta mchanga tu, nataka nikwambie ukweli, hujanifurahisha, nataka kuanzia wiki ijayo ujenzi huu uende haraka na ukamilike mapema.
“Nawashukuru IGP na Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kunialika kwenye shughuli hii ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 118 za askari wa Jeshi la Polisi hapa Dodoma. Nitoe wito kwa wanaotekeleza mradi wa ujenzi huu wafanye haraka na mmeniahidi kuwa utakamilika kwa wakati na iwe hivyo ili askari wangu wapate sehemu nzuri ya kukaa.
“Ndugu zangu Askari endeleeni kuchapa kazi, ili Tanzania na watu wake waendelee kukaa kwa amani, mimi nipo pamoja na ninyi, endeleeni kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu mkubwa, Watanzania wanawategemea ninyi.
Comments are closed.