The House of Favourite Newspapers

Kamwamba: Chichi Mawe Hamalizi Raundi 10

0

Israel Kamwamba – Malawi.

 

ISRAEL Kamwamba raia wa Malawi ni mpinzani wa Francis Miyeusho ‘Chichi Mawe’ ambaye anarekodi ya kucheza mapambano nane na yote ameshinda, matano yakiwa kwa KO, rekodi zi­naonyesha ni moto wa kuotea mbali kufuatia kukaa juu ya ringi kwa raundi 34.

 

Mabondia wengine watakaopanda ulin­goni Julai 22, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Dar Live ni Nasibu Ramadhan ‘Pacman’ atakayezichapa na Benard Mwango wa Zambia wakati Idd Pi­alali atapanda ulingoni dhidi ya Regin Cham­pioni kutoka DR Congo.

Utamu wa mapambano hayo ambayo yatarushwa mubashara na kituo cha Global TV Online hasa kwa upande wa Kamwamba na Chichi Mawe unatokana na utofauti wa staili ya miguu wanaoyotumia mabondia hao, Chichi Mawe ni south­paw yaani anatanguliza mguu wa kulia mbele.

Francis Miyeusho ‘Chichi Mawe’ -Tanzania.

 

Wakati Kamwamba ‘Israiel Mweusi’ ni orthodox yaani ana­tanguliza mguu wa kushoto mbele, hivyo hapo ushindani wa kimataifa utaonekana kabisa kwa kuwa kila mmoja anahitaji ku­chukua ubingwa huo wa Global TV, Afrika Mashariki na Kati.

Katika mapambano hayo ya kimataifa, yaliyoandaliwa na Kampuni ya Solid Rock Tan­zania, yatasimamiwa na Ka­misheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) chini ya rais wake, Yassin Abdallah ‘Us­taadh’.

Kamwamba katika mas­umbwi hayo yatakayorushwa mushabara na Global TV Online kupitia tovuti yake ya www.glo­baltvtz.com amefanya mahojiano maalum na Championi Ijumaa na kueleza maandalizi yake kuelekea pambano hilo.

Regin Champion – Congo.

 

 

“Na jiandaa vizuri, nataka kazi yangu iwe ya heshi­ma hasa ni kuhakikisha napata ushindi wa aina yake.

“Natambua kuwa nakuja Tanzania kwa ajili ya pambano langu dhidi ya Francis Miy­eyusho ni pambano langu la kwanza kubwa la ubingwa ndani ya Tanza­nia.

“Nalipa nafasi ya umuhimu na uku­bwa wake ili niweze kuonye­sha kipaji na ubora wangu la­kini vilev­ile litani­weka katika rama ni ya dunia.

Nasibu Ramadhan ‘Pacman’ -Tanzania

 

 

“Siyo kitu kidogo kwangu ku­timiza hilo li­cha kuwa ya meneja wangu hufanya kazi mara kibao na mabondia wa Tanzania kama Francis na Cosmas Cheka na Jay Msangi, kwangu ni kitu cha heshima.

“Naamini pambano litakuwa zuri kutokana na maandalizi ambayo naendelea kuyafanya chini ya uon­gozi wangu, nina rekodi nzuri japo mpinzani wangu kidogo amenizidi ila siwezi kumuhofia.

“Ngumi ndiyo zinanileta Tanzania sasa siwezi kuzembea hasa kuto­kana na ukubwa wa rekodi yake, kwangu vita popote haijalishi nipo wapi hivyo nitakuja kwa ajili ya ku­pigana na siyo kucheza Chess.

Idd Pialali – Tanzania.

 

“Kiukweli niwashukuru waandaaji Global TV Oline kwa hatua hii kubwa ambayo wameamua kui­fanya kwa sababu mabondia wapo wengi ila nimechaguliwa mimi, ni kitu cha kujivunia.

“Kutokana na maandalizi am­bayo naendelea kuyafanya ni makali kwa kuwa mmoja kati ya mabondia ambao nafanya nao mazoezi yeye atakuwa akielekea Kosovo.

“Watanzania wajue kuwa naku­ja kumaliza utawala wa Miyey­usho kwa sababu siogopi uzoefu wake wa muda mrefu aliokuwa nao tena asipokuwa makini nita­mpiga kabla ya raundi ya nane.

Mikanda ya ubingwa wa Global TV Online.

 

 

UNAWAAMBIAJE MASHABIKI WA MALAWI KWA KUWA GLOBAL TV ONLINE WATARUSHA LIVE?

“Hiki ni kitu kizuri kwangu na kwao kwa sababu wataweza kuona kazi nitakayokuwa naifanya ulingoni na kujua ubora wa kiwango changu.

Global TV itawasaidia ndugu zangu na mashabiki nchini kwetu kuweza kuniona wakati nikicheza na nitawaambia mapema njia yao wa kuweza kuona katika chaneli ya Global TV ambayo inapatikana YouTube.

“Wao wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwanza wanaingia YouTube na kujiunga (subscribe) katika chaneli ya Global TV Online,” anasema Kamwamba.

 

Katika hatua nyingine Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdallah ‘Ustaadh’ alisema pambano hilo, halitakuwa na kiingilio na mashabiki wataweza kulishuhudia mubashara kupitia simu zao za mkononi tu, kwani litaonyeshwa na Global TV pekee. Wadau na mashabiki wa­takaopata nafasi ya kuingia ukum­bini wataingia kwa kadi maalum za mwaliko tu.

 

Ustaadh aliongeza: “Ili kulishuhu­dia pambano hilo kwa njia ya simu tena bure, hakikisha unajiunga na YouTube chaneli ya Global TV Online sasa hivi ili usipitwe. Ingia YouTube, tafuta GLOBAL TV ONLINE, kisha bonyeza neno subscribe pia bonye­za kikengele kidogo kilichopo pem­beni yake ambacho kitakukumbu­sha kuangalia pambano hilo mara tu litakapoanza.

 

“Kama wewe ambaye umeshajiun­ga, basi hakikisha pia umebonyeza kikengele ili usipitwe na kila kina­choendelea Global TV. Pia unaweza kuwapata kupitia mtandao wa www. globaltvtz.com, jiunge sasa na Glo­bal TV ili uwe wa kwanza kuona ndondi za kimataifa siku hiyo. Ka­jiunge sasa kwa kuingia www. youtube.com/user/uwazi1” alisema Ustaadh.

 

IBRAHIM MUSSA |  GLOBAL PUBLISHERS

WATAKAOCHUANA HAWA HAPA

Leave A Reply