Kibarua cha Kocha Ndayiragije Chaota Nyasi Stars
SHIRIKISHO soka nchini, (TFF) leo Februari 11, 2021, limekubaliana kuvunja makubaliano na Kocha wa Taifa Stars, Etienne Ndayiragije. Hii ni baada ya makubaliano ya kikao cha pamoja.
Katika taarifa yake, TFF imeshumkuru Ndayiragije kwa kazi yake akiifundisha Stars na kumtakia mafanikio mema aendako.
Aidha, TFF imesema itamtangaza mbadala wake baada ya mchakato wa kumpata utakapokamilika.