The House of Favourite Newspapers

Kocha Simba Afungukia Sakata Lake Na Morrison

0

DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa taarifa ambazo zinaeleza kwamba ana ugomvi na mchezaji wake Bernard Morrison zimemsikitisha kwa kuwa wanaishi wakiwa ni familia ndani ya timu.

 

 

Hivi karibuni imekuwa ikielezwa kuwa kocha huyo raia wa Ufaransa hawaivi chungu kimoja na Morrison jambo ambalo lilimfanya amuweke kando kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania ambao ulikuwa ni wa ligi.

 

 

 

Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, ubao ulisoma Simba 3-0 JKT Tanzania baada ya dakika 90 na nyota huyo hakuanza kwenye mchezo huo.

 

 

 

Pia kwenye msafara wa Simba ambao uliibukia nchini Sudan kumenyana na Al Merrikh mchezo uliochezwa Machi 6 na ubao kusoma Al Merrikh 0-0 Simba baada ya dakika 90, Morrison aliachwa Bongo.

 

 

 

Gomes amesema: “Kuhusu kuwa na ugomvi ni Morrison pamoja na kutoelewana nayo hiyo sio kweli kwa kuwa nimekuwa nikizungumza naye vizuri.

 

 

“Pia sisi tunaishi tukiwa ni familia hakuna ambaye anamkasirikia mwenzanke, kuhusu kubaki hilo siwezi kutaja sababu kwa kuwa mwalimu anajua aina ya wachezaji ambao anawahitaji ila hakuna ugomvi kati yangu na Morrison,” .

 

 

Morrison aliibuka ndani ya Simba akitokea Klabu ya Yanga ambapo amekuwa hana nafasi kikosi cha kwanza ndani ya Simba tangu zama za Sven Vandenbroeck ambaye alibwaga manyanga.

Leave A Reply