Kuvimba kwa matiti ukinyonyesha
Wanawake wengi wanapokuwa kwenye uzazi husumbuliwa na kuvimba kwa matiti hasa pale wanapokuwa wananyonyesha, leo nawaletea tiba inayosaidia kumaliza tatizo hilo mzazi anapogundua uvimbe.
Hali hiyo humsababishia mama kushindwa kumnyonyesha mtoto wake kwani ziwa hutoa maji badala ya maziwa huku likiambatana na maumivu makali.
Kunywa maji mengi
Kunywa maji mengi husaidia tatizo hili kupungua, cha kufanya wakati unanyonyesha jitahidiĀ kuweka maji pembeni yako kila wakati, kwa kunywa maji hayo kwa wingi husaidia kuondoa maambukizi.
Vitunguu swaumu :
Kitunguu swaumu si kizuri kwa mtoto lakini kama unanyonyesha na tatizo hilo limekupata, unaweza kukitumia kwani kinasaidia kuondoa maambukizi yanayoshambulia ziwa.
Unaweza kukitumia kwa kumeza kila siku punje moja au kutumia kwenye chakula chako ili kuweka ulinzi wa bakteria kutokukushambulia.
ITAENDELEA WIKI IJAYO