Kongamano hilo ambalo limeandaliwa na Taasisi ya Vijana Wazalendo wa Kitanzania – Tanzania Youth Patriots (TYP), limefanyika kuanzia saa 7:00 mchana ambapo wazungumzaji wote walipata fursa ya kutoa maoni yao kuhusu uzalendo na namna ya kuwa mzalendo katika nchi ya Tanzania.
Wazungumzaji waliokuwepo ni;
Mgeni Rasmi ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Makamba.
Mgeni wa Heshima ni Mtangazaji wa Kimataifa kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika (VOA) ambaye ni mhariri wa idara hiyo na mtangazaji wa Kipindi cha Straight Talk Africa, Shaka Ssali.
Watoa mada ni Maria Sarungi Tsehai, Lawrence Masha, Eric Shigongo, Mzee Shaba na Benjamin Fernandes.