The House of Favourite Newspapers

JPM Aendesha Basi la Mwendokasi, Awaagiza Simbachawene na Mbarawa Kufikia Jioni Wampe Ripoti ya Makusanyo ya Mradi

magufuli-mwendokasi-10       

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia mkono pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop mara baada ya kutoka kukagua moja ya basi linalotumika katika utoaji huduma ya Usafiri wa Haraka (BRT)

Hapa nimekuwekea mlolongo wa matukio, hatua kwa hatua wakati Rais Magufuli alipozindua Rasmi Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka awamu ya kwanza, hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Gerezani vilivyopo maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam leo Jumatano, Januari 25, 2017 mchana.

: Mgeni Rasmi, Rais Magufuli ameshawasili kwenye hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar (UDART) awamu ya kwanza inayofanyikia Kariakoo, Gerezani, Dar.

makamu-wa-rais-benki-kuu

Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Mhe. Makhtar Diop akiongea machache kwenye sherehe za ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar.

: Mradi ukikamilika utaweza kujiendesha bila kuhitaji ruzuku kutoka serikalini. -Simbachawene

: Live Kutoka Kariakoo, JPM Akizindua Rasmi wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi DSM.

magufuli-mwendokasi

 Rais Magufuli akiongea na Diop kwenye sherehe hizo.

: Endapo mradi huu utakamilika ipasavyo, UDART itakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 450,000 kwa siku.- Waziri Simbachawene.

Madhumuni ya Mradi huu ni kushusha kiwango cha nauli ili Watanzania waweze kutumia usafiri huu. Waziri Simbachawene.magufuli-mwendokasi-3

 Rais Magufuli akiweka kadi ya Kieletroniki katika Mashine ya UDART ilikuweza kupita kama ishara ya Ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Pembeni yake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene akimuelekeza jambo katika mashine hizo.

: Kiwango cha nauli kushuka Mradi kuweza kujiendesha bila kuhitaji ruzuku kutoka serikalini. – Waziri Simbachawene.

:  Serikali inamiliki asilimia 49 za hisa wakati Kampuni ya Simon Group inamiliki 51 za UDA. – Waziri Simbachawene.

AWAMU ZA UJENZI WA UDART

Awamu ya 1- Kimara Kivukoni, Magomeni hadi Moroko, Kariakoo

Awamu ya 2: Barabara ya Kilwa hadi Gerezani na Mbagala Rangi Tatu, fly overs kati ya Chang’ombe na Uhasibu.magufuli-mwendokasi-8

 Rais Magufuli akifurahia mara baada ya kuendesha gari la Mwendo Kasi katika kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Haraka (BRT) mara baada ya kufungua rasmi Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.

Awamu ya 3- Barabara ya Nyerere, Uhuru, Bibi Titi na Azikiwe katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongo la Mboto.

Awamu ya 4. Bibi Titi, Sam Nujoma na Nyerere.

Awamu ya 5. Barabara ya Mandela.

Awamu ya 6. Barabara ya Mwai Kibaki.- Amesema Waziri wa Ujenzi, Prof. Makame Mbarawa.magufuli-mwendokasi-7

  Rais Magufuli akipunga mkono kwa wanahabari mara baada ya kuzindua utoaji huo wa huduma ya usafiri.

: Rais Magufuli amesema mkandarasi wa kwanza wa Mradi wa Mwendokasi alikuwa Mchina, alishindwa akatumbuliwa akaondoka ndipo akaletwa Strasburg wa Ujerumani.

: Rais Magufuli aiagiza Wizara ya Ujenzi kushughulikia changamoto iliyoko Makutano ya Barabara Ubungo Mataa ili kufanikisha Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka.

: Rais Magufuli awaagiza Mawaziri George Simbachawene wa TAMISEMI na Prof. Makame Mbarawa wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi pamoja na wasimamizi wa mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dara, kufikia leo jioni wampe ripoti inayoonesha kiasi cha fedha iliyopatikana kama faida kwenye mradi huo.magufuli-mwendokasi-6

 Rais Magufuli akipita kwenye mashine hizo mara baada ya uzinduzi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.

‘Mawaziri mmetoa taarifa nzuri lakini mmeninyima raha kwa kotonipa taarifa ya pesa mlizotengeneza kutokana na mradi huu’

‘Nilitaka nijue kama mradi umetengeneza faida basi ningetoa maagizo Kimara pajengwe kituo kikubwa cha maegesho ya magari’

‘Nawaagiza kufikia leo jioni muwe mmenipatia ripoti ya kiasi cha faida kilichopatikana tangu mradi huu uanze ili nijue kama kuna faida au hasara, kama ripoti mnazo mnipe hapa sasa hivi.’ Alisema Rais Magufuli.magufuli-mwendokasi-5

 Rais Magufuli akipita kwenye mashine hizo.

: Rais Magufuli amependekeza kujengwa kwa kituo kikubwa cha maegesho ya magari ya daradala na madogo madogo eneo la Kimara ili kuvutia watu ambao wakishuka kwenye magari yao binafsi ama daladala wapande ya mwendokasi, au wakishuka mabasi ya mwendokasi iwe rahisi kupanda daladala au magari yao binafsi.

‘Wapo watu wanatoka na magari yao wanapofika Kimara wanataka watumie mabasi ya haraka lazima kuwe na eneo la parking ya magari’magufuli-mwendokasi-4

 Rais na Diop pamoja na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar.

‘Tumepanga kujenga barabara za juu kwenye makutano ya barabara DSM na kujenga daraja litakaloanzia Coco Beach mpaka Hospitali ya Aga Khan.”

“Miradi ya mabasi ya haraka ktk Afrika ipo Nigeria na Afrika Kusini lakini miradi hiyo sio mikubwa kama huu wa Tanzania.” Alisema Rais Magufulimagufuli-mwendokasi-1

 Rais Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wa kwanza kulia wavivuta kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene pamoja na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.


: Rais Magufuli awaagiza vikosi vya Usalama Barabarani kuwashughulikia wanaoingiza magari kwenye njia za mwendokasi kwani wanavunja sheria za nchi. Ameagiza wakamatwe na kupelekwa vituo vya polisi ama kung’oa mataili kwenye magari yao ili liwe fundisho kwao na kwa wengine.

‘Trafiki mkiona pikipiki, gari linatumia barabara hizi za mwendokasi yashikeni pelekeni kituo cha polisi, yatoeni matairi ili wajifunze’

“Saa nyingine ukitumia sheria tu watu hawajifunzi lazima mtumie nguvu za ziada ili waziogope hizo barabara za mwendokasi.Alisema Rais Magufuli.magufuli-mwendokasi-2

 Rais Magufuli akipiga makofi pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wakwanza (kulia) akivuta utepe kuashiria Ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.


#UzinduziwaBRT: Rais Magufuli amezindua Rasmi Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka, awamu ya kwanza katika Viwanja vya Gerezani vilivyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam.

#UzinduziwaBRT: Rais Magufuli amezindua rasmi Miundo Mbinu ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka, awamu ya kwanza katika Viwanja vya Gerezani, Kariakoo jijini Dar.

#UzinduziwaBRT: Rais Magufuli ameendesha moja ya mabasi ya mwendokasi wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi, Viwanja vya Gerezani, Kariakoo jijini Dar.magufuli-mwendokasi-9

 

#UzinduziwaBRT: Akizungumza kuhusu utekelezwaji na uboreshwaji wa Mradi wa Mabasi Yendayo Haraka jijini Dar, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema ametoa agizo kwa wamachinga wote wanaofanya kazi zao kandokando ya barabara za mabasi ya mwendokasi waondoke wenyewe kulekea kwenye maeneo waliyotengewa ambayo moja wapo ni Mtaa wa Lumumba kabla ya Manispaa yake haijachukua hatua za kuwaondoa kwa nguvu.

magufuli-mwendokasi-11

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wakati Msanii Mrisho Mpoto alipokuwa akitumbuiza.

PICHA NA IKULU

#UzinduziwaBRT: Naye Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene ameongeza kuwa wmachinga wanaofanya biashara zao kwenye njia za waenda kwa miguu waondoke mara moja kwani wanavunja sheria na kusababisha madhara na hata watembea kwa miguu kugongwa na magari na kufa.

Rais Magufuli Aendesha Basi la Mwendokasi Mwenyewe

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam

Comments are closed.