The House of Favourite Newspapers

Lolly Pop: Moyo Mashine haukuwa wa Barakah Da Prince

0

Goodluck GozbertGoodluck Gozbert.

PRODYUZA na muimbaji wa nyimbo za Injili, Goodluck Gozbert ‘Lolly Pop’ amezima tetesi zilizozagaa kuwa wimbo mpya wa Bernad Paul ‘Ben Pol’ wa Moyo Mashine ulikuwa umeandikwa maalum kwa msanii, Baraka Andrew ‘Barakah Da Prince’ kuwa si kweli.

ben poloBernad Paul ‘Ben Pol’

Akigonga stori mbili-tatu na mtandao huu, Lolly Pop ambaye amehusika katika kumwandikia mashairi nyimbo karibu zote za Barakah alisema kuwa Wimbo wa Moyo Mashine aliuandika mwaka jana na ulikuwa mahususi kwa Ben Pol.

baraka prince (2)Barakah Da Prince

“Si kweli kama nimempa wimbo Ben Pol badala ya Barakah. Kwanza Moyo Mashine imepikwa na maprodyuza watatu yaani mimi Kidboy na Nasder timu ambayo ilikuwa ikifanya kazi na Barakah huenda watu wameliona hilo na kuanza kuongea yao,” alisema Lolly Pop.

Leave A Reply