The House of Favourite Newspapers

Lori Nusura Liue Watu Ubungo – Video

0

LORI la mizigo aina ya Scania lenye namba za usajili T 106 DKD nusura liue watu baada ya kutokea ajali katika eneo la Ubungo External, Barabara ya Ubungo – Mwenge jijini Dar es Salaam leo Ijumaa, Juni 4, 2021.

 

Kwa mujibu wa dereva wa gari hilo amesema kuwa, kuna raia mmoja aliyekatisha ghafla kwenye zebra wakati taa zimeruhusu magari yapite hali iliyosababisha dereva wa hiace aliyekuwa mbele kufunga brake ghafla.

 

Baada ya dereva hiace kufunga brake, dereva wa lori aliyekuwa nyuma ya hiace hiyo alilazimika kuikwepa hiace ili asiigonge kwani asingeweza kufunga brake ya haraka kutoka na mzigo mkubwa aliokuwa amebeba na pengine angesababisha vifo vya abiria wote walikuwemo ndani ya hiace hiyo…..

Hali ndio kama inavyoonekana hapa.

cc: Ripota wa Mtaani @gabby_mtanzania255
@globaltvonline
@255globalradio

 

View this post on Instagram

 

A post shared by Global Publishers (@globalpublishers)

Leave A Reply