The House of Favourite Newspapers

Lucy Komba Atamani Mwanaye Angekuwa Mzungu

0

 

Msanii wa filamu Lucy Komba.

MSANII wa filamu Lucy Komba amese­ma, anajivunia kuona mtoto wake anayeishi naye nchini Denmark kwa mumewe, kuweza kuongea lugha ya Kingereza na kusahau kabisa Kiswahili.

Akipiga Stori na 3-Tamu, Lucy alisema moja ya vitu vilivyo­mfanya akaishi huko na mwa­naye ambaye si mtoto wa Mzungu huyo ni kutaka awe na tabia za Kizungu ikiwemo kujua lugha hiyo kwa ufasaha ili kuon­dokana na mambo mengi ya Kiswahili, ikiwemo kumsomeshe nchi za Wa­zungu hadi pale atakapo­hitimu elimu ya juu.

Lucy komba akiendelea na mtoto wake.

“Kitambo nawaza male­zi bora kwa mwanangu, sikupenda awe na tabia za Kibongo japo ni Mbongo, hivi sasa siyo yeye kabisa ameshasahau Kiswahili siku nyingi maana mtoto anan­asa kirahisi, nimefurahi mno,” alisema Lucy ambaye mtoto wake anayeit­wa Strom anaishi naye huko zaidi ya mwaka sasa.

STORI: MAYASA MARIWATA | AMANI

Shuhudia Watoto Waliozaliwa Wameungana Moro, Baba Aomba Msaada

 

Leave A Reply