Lulu: Sichukii baby wangu kuwa na watoto baki
Stori: IMELDA MTEMA
Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amewakata ‘vilimi’ wale waliokuwa wanamsema vibaya kuhusu mchumba wake kuwa na watoto wakubwa aliozaa na wanawake wengine.
Akistorisha mawili matatu na paparazi wetu, Lulu ambaye yupo penzini na baby wake huyo ambaye ni bosi wa redio maarufu Bongo (jina kapuni), alisema anachokiangalia kwake ni mapenzi ya dhati waliyonayo, haijalishi huko nyuma mpenzi wake kuwa na watoto watatu.
“Sina kinyongo, nawapenda wanawe kama ninavyompenda yeye. Sioni tatizo kutembea nao popote maana Mungu akijalia nami nitapata wangu, ” alisema Lulu.