Magufuli amwaga sera ya matumaini mapya Singida
Capt Mstaaf, John Chiligati aliyekuwa Mbuge wa Manyoni akipunga mikono baada ya kumpigia debe mgombea mpya ubunge wa jimbo hilo, Daniel Mtuka.
Chege na Temba wakikamua.
Magufuli (kulia) akimsiliza kwa tabasamu Wazir wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu kwenye viwanja vya Itigi, mkoani Singida.
Magufuli akimwaga sera kwa wakazi wa Itigi, Singida
Magufuli akimwaga sera kwa wakazi wa Kilimatinde mkoani Singida, walipomsimamisha barabarani akiwa anapita eneo hilo.
Magufuli akiomba kura kura kutoka kwa wakazi wa Bahi sambamba na mgombea ubunge jimbo hilo, Baduel.
Magufuli akiongea barabarani na wakazi wa Puma, Singida baada ya kundi la wakazi hao kumsimamisha wakati akipita.
Magufuli akiwasalimia wanachadema wa Manyoni na kuwataka wampigie kura yeye na mbunge wake Daniel Mutuka.
Magufuli alivyowasili Itigi.
Magufuli akizungumza na wakazi wa Ikungi, Singida Mashariki
Makomandoo wa Kibega wakikamua viwanja vya Ikungi mnadani.
Akinamama wa manyoni wakiwa kwenye shamrashamra za kumkaribisha Dk john Magufuli.
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) John Magufuli, leo alimwaga sera katika Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma na kuingia Mkoa wa Singida ambapo alifanya mikutano kwenye vijiji miji ya Chikuyu, Kilimatinde, Manyoni, Itigi, na kumalizia na Itigi iliyopo Jimbo la Singida Mashariki.
Katika mikutano hiyo Magufuli aliitangaza ilani ya utekelezaji ya chama chake ambayo inatoa kipaumbele kwa mambo kadhaa ikiwemo kupunguza shida ya maji safi na salama, huduma za afya, barabara, kupunguza ushuru kwa wafanyabiashara wadogowadogo na wakubwa, kutoa mikopo kwa ajili ya mitaji, elimu bure na mengine mengi.
Akimwaga sera hizo Magufuli alitoa ufafanuzi wa jinsi atakavyoiteleza ilani hiyo hali iliyosababisha kila alitoa ufafanuzi watu wamshangilie kwa vifijo na nderemo.
HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPLÂ Â