The House of Favourite Newspapers

Makamu wa Rais Mpango: Mitambo Miwili ya Kuzalisha umeme katika Bwawa la JNHPP Itawashwa

0

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Philip Mpango akizungumza na wananchi wa Kabuku Wilaya ya Handeni wakati akiwa ziarani mkoani Tanga tarehe 21 Februari 2024.

Makamu wa Rais Dk Philip Mpango, amesema mwezi Machi mwaka huu itawashwa mitambo miwili ya kuzalisha umeme katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP), ambayo itasaidia kumaliza makali ya changamoto ya ukosefu wa umeme nchini.

Amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Kabuku wilayani Handeni, akiwa njiani mkoani Taga ikiwa ni ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

Amesema walikuwa wamejipanga kuwasha mtambo mmoja mwezi huu, lakini wameona ni vyema wasubiri mpaka mwezi ujao, ndio waweze kuwasha mitambo miwili ambayo itaimarisha hali ya upatikanaji wa huduma hiyo.

“Ule mradi wetu wa kuzalisha umeme, umefikia hatua nzuri, ilikuwa tufungue mtambo mmoja lakini sasa tunakwenda kufungua mitambo miwili toka kwenye bwawa letu jipya,”amesema Dk Mpango.

Leave A Reply